Friday, 27 May 2016

Rais Obama atembelea mji wa Hiroshima


Rais Obama atembelea mji wa Hiroshima

  • siku ya leo
 
Image caption Obama akiwa Japan
Rais Barrack Obama amekuwa rais wa kwanza aliye mamlakani nchini Marekani kutembelea mji wa Hiroshima tangu shambulio la nuklia wakati wa vita vya pili vya dunia.
Obama amesema kuwa kumbukumbu za tarehe 6 mwezi Agosti 1945 hazifai kusahaulika,lakini hakuomba msamaha wa shambulio hilo la Marekani ikiwa ni bomu la kwanza la kinyuklia kutumika duniani.
Image copyright Reuters
 
 
Image caption Obama akiwasili mjini Hiroshima
Bw Obama alizungumza na baadhi ya walionusurika na katika hotuba yake akayataka mataifa kujiendeleza bila silaha za kinuklia.
Takriban watu 140,000 walifariki mjini Hiroshima na wengine 74,000 siku mbili baadaye katika bomu la pili katika mji wa Nagasaki.
Image copyright AFP
 
Image caption Obama akiweka shada la maua katika makavazi ya kumbukumbu ya Hiroshima
Bw Obama alitembelea makavazi ya Heroshima kabla ya kuelekea katika eneo la kuhifadhi kumbukumbu za shambulio hilo,akiandamana na waziri mkuu Shinzo Abe.Wote wawili walisimama mbele ya mwanga wa milele.

Hiroshima memory must never fade, Obama says on historic visit

 Barack Obama has become the first serving US
president to visit Hiroshima since the World War Two nuclear attack.
Mr Obama said the memory of 6 August 1945 must never fade, but did not apologise for the US attack - the world's first nuclear bombing.
Mr Obama spoke to two survivors and in an address called on nations to pursue a world without nuclear weapons.
At least 140,000 people died in Hiroshima and another 74,000 three days later in a second bombing in Nagasaki.
 Barack Obama, 27 May, Iwakuni base

Media captionDuring an address Mr Obama called on nations to pursue a world without nuclear weapons
Media captionDuring an address Mr Obama called on nations to pursue a world without nuclear weapons

'Best of friends'

Mr Obama first visited the Hiroshima Peace Memorial Museum before walking to the Peace Memorial Park, accompanied by Prime Minister Shinzo Abe.
Both men stood in front of the eternal flame. Mr Obama laid a wreath first, followed by Mr Abe.

The bomb that changed the world


"Death fell from the sky and the world was changed," Mr Obama said in his address, noting that the bombing had shown that "mankind possessed the means to destroy itself".
Mr Obama said the memory of Hiroshima must never fade: "It allows us to fight complacencies, fuels our moral imagination and allows us to change."
Of nuclear weapons, he said: "We must have the courage to escape the logic of fear and pursue a world without them."
Mr Obama then spoke to two survivors, hugging 79-year-old Shigeaki Mori.
"The president gestured as if he was going to give me a hug, so we hugged," Mr Mori said.
Mr Obama also talked to Sunao Tsuboi, 91.

Symbols and codes - BBC's John Sudworth in Hiroshima

The image of President Obama hugging a survivor will resonate deeply with the Japanese public. Opinion polls show that the majority of people welcome this visit and most, it seems, do not mind either about the absence of an apology.
The deep symbolism is enough; the leader of the only country ever to have used an atomic weapon laying a wreath in a city that has become a monument to the perils of our nuclear age.
But others will point out that, while his speech was long on lofty idealism, he remains the commander in chief of one of the world's largest nuclear arsenals, one that he has approved billions of dollars to modernise.
Standing just a few rows away from the president, as he always does, an officer could be seen holding the briefcase containing the nuclear launch codes.
Image copyright AFP
Image caption The nuclear code briefcases loaded at the White House for the Asian trip

Mr Obama had earlier flown into the nearby Iwakuni Marine Corp base nearby, after leaving the G7 summit.
Mr Obama told service personnel at the base: "This is an opportunity to honour the memory of all who were lost during World War Two."
Mr Obama praised the US-Japan alliance as "one of the strongest in the world", with his visit "a testament to how even the most painful divides can be bridged - how our two nations, former adversaries, cannot just become partners, but become the best of friends and the strongest of allies".
Image copyright AFP
Image caption Mr Obama and Mr Abe both laid wreaths at the Peace Memorial Park
Image copyright AFP
Image caption Mr Obama praised US troops for their sacrifices, in his speech at the Iwakuni marine base
Many in the US believe the use of the nuclear bomb, though devastating, was right, because it forced Japan to surrender, bringing an end to World War Two.
The daughter of one survivor, who was visiting the memorial on Friday, said the suffering had "carried on over the generations".
"That is what I want President Obama to know," Han Jeong-soon, 58, told the Associated Press news agency. "I want him to understand our sufferings."
Seiki Sato, whose father was orphaned by the bomb, told the New York Times: "We Japanese did terrible, terrible things all over Asia. That is true. And we Japanese should say we are sorry because we are so ashamed, and we have not apologised sincerely to all these Asian countries. But the dropping of the atomic bomb was completely evil."
You need to install Flash Player to play this content.
Media captionFilmmaker Barry Frechette told Shigeaki Mori's story in the film Paper Lanterns
You need to install Flash Player to play this content.
Media captionWhat happened after the US atomic bombs and why President Obama's visit matters
China responded to the visit by saying that Japan's six-week attack on the Chinese city of Nanjing, which began in December 1937, was more worthy of reflection.
The Chinese say 300,000 people were killed, although other sources say the figure was lower.
"Victims deserve sympathy, but perpetrators should never shirk their responsibility," Chinese Foreign Minister Wang Yi said.

'Just listen' - Japan's media on the visit

The Chugoku Shimbun urges Mr Obama to "hear the voices of Hiroshima". "The people of Hiroshima will be watching the president closely, eyeing to what extent he is truly resolved to advance the abolition of nuclear arms," it said.
The Asahi Shimbun carries an article saying Mr Obama's "gestures will shape the visit", with the "most powerful gesture" being to "just listen to the bomb victims' memories of suffering and activism".
The Japan Times says: "To truly pay homage to those whose lives were lost or irrevocably altered by the Hiroshima and Nagasaki bombings, Obama's visit must galvanise the international community to move without delay toward a world free of nuclear weapons. The fact that these weapons have not been used over the past 70 years does not guarantee a risk-free future for our children."
Source: BBC Monitoring

Hiroshima - world's first nuclear attack

SUCCESS IS YOURS





I want to share with you five steps on how to reach your GOALS .We all want specific things in our life, the problem is how to reach what we desire. It’s not always easy to reach our goals, but are there any tricks to reach them? There aren’t any easy answers to that question, however I have a few ideas that might help you get there:

         1- Believe in yourself
. I cannot put enough emphasis on the fact you need to believe in yourself and in your abilities to achieve anything in life. Believing in yourself is the key to almost everything you will start. If you start a business not only you need to be in love with what you do, but you also need to believe in the fact it can work. It’s the stepping stone to any foundation. Most of us already do this for common things like cooking, driving a car or taking a class in University.
   2- Think about the process to reach your goal
Planning ahead is important, especially when you are trying to reach a specific goal. It’s very important to visualize each of the steps needed to reach your goals. Imagine yourself doing these steps, living each instant of them. This is a very easy way to plan ahead, it also helps you not forget anything along the way. By visualizing the steps you can see what you need to do to reach your goals. When the time arrives and you are living those steps, you will probably get achievement and this comes from the fact you already imagined it. I usually do this before going to bed, which brings me to my third point.
    3- Visualize your steps before going to bed
Yes, visualizing each steps before going to bed will not only help you reach you goals with less hurdles it will also make you dream about it. I often dream about my goals or my daily life, this gives me practice in what I am about to do. Did you know when you sleep your brain doesn’t know the difference between reality and fiction? This explains why your dreams can feel so true. It also explains why a nightmare can feel so real. Once we understand this concept you can see all the advantages of dreaming properly. I will write a post another post soon dedicated to this technique.
     4- Strive, fight and stay positive
Your goals won’t happen overnight, they also won’t happen without work. You will have to overcome many obstacles before you reach your desired goal. There are always people who will work against you (if it’s not yourself doing so) or technical hurdles you will need to overcome. NEVER discourage yourself, always stay positive and focus on being a problem solver. Keep pushing and never discourage yourself even when you think everything is lost. No one has ever achieved anything without past failures or setbacks, try to stay positive.
       5- Get backup, use your contacts and talk to people
Don’t be shy to talk to people about your new goals and how you plan to achieve them. Other people’s insight can be very important and can help skip a few steps. A teacher once told me that on a construction yard do they build new trucks and tools for each new construction? The answer is NO.    The same concept applies to our life and experiences, you can use other peoples experiences to learn quicker and get by some of the steps. (In this example they are your tools) This can be true on tangibles goals like setting up a business, going back to school or building by yourself a shed in the backyard. Getting help is not only smart and quicker it will also show your friends and family that you want to learn and achieve your goals.
       I want to point out one important thing about goal setting. I believe anything is possible and that everyone can reach their goals. Keep in mind some goals might not be possible to achieve. We need to be realistic in life, I understand this only applies to 1% of population, but common sense is important (after all, this is a blog for logical people ). Also if you set your goals too high you will be disappointed if you can’t reach them appropriately, so don’t be too greedy and make sure whatever your goal is, that deep down inside, that is what you really want.

Did you like this article? Why don't you share it via Facebook, Twitter, Google+, StumbleUpon, or any other way you want!
     Prepared by: Elisante Daudi
     Contact No: +255759762229
     Email       EDYoramu@gmail.com
    Facebook: Elisante Daudi
 
 

Monday, 23 May 2016

JIPATIE KIPATO KWA BIASHARA YA MAUA

FUMBUA MACHO UONE MBINU ZA KUPATA FEDHA KWA KUUZA MAUA

Kumekuwa na manunguniko kati ya watu wengi wakiwaza watatumia njia gani kutengeneza fedha, napenda kukupa elimu na mbinu za kujipatia na kujiongezea kipato kwa njia ya uuzaji wa maua.

                      Hakuna mtu asiyependa maua, maua hutumika kama kivutio kikubwa cha maeneo mbalimbali ,kila nyumba utakayo itembelea utakuta maua ndani ya nyumba au nje ya nyumba,kila sherehe au kumbi za mikutano utakuta maua hii ni ishara tosha kuwa maua ni mhimu na yanahitajika.
Hakuna nchi isiyo hitaji maua tena kumekuwa na wafanya biashara ambao wamekuwa wakisambaza bidhaa zao nje,mataifa makubwa na madogo duniani yanahitaji kuona maua . 
Napenda kukuhamasisha uone umhimu wa biashara hii kwani haitaji mtaji mkubwa ni mtaji wa kawaida ila muda na nguvu kwanini nakuambia haihitaji mtaji mkubwa?
Nimekuambia haitaji mtaji mkubwa kwa sababu ifutayo:
Zipo mbengu za maua ambazo hupatikana kwa uurahisi kazi yako inakuwa kupandikiza au kuotesha .
Faida za uuzaji maua     
Zipo faida mbali mbali unazoweza nufaika nazo kwa biashara hiyo mfano unaweza kuzarisha miche elfu moja na kila mche unaweza kuuza kwa bei tofauti kulingana na hadhi ya ua lenyewe, jaribu uchukulie bei ya sh,500 kwa mche na uzalishe miche 1000 utapata kiasi cha sh,500000/= kumbuka hiyo ni bei ya makadirio ya chini waza kwa yale maua yanayouzwa mche 1500 na kuendelea.
Nalotaka kukuhamasisha zingatia yafuatayo muda wakupandikiza miche hauzidi mwezi hadi miezi miwili lakini zikisha ota tayari unauhakika wa kuvuna fedha.
 Huenda wewe ni mfanya biashara ya maua na unapenda nikutafutie soko la maua yako usisite kuwasiliana nami kwa namba zinazopatikana kwenye blog hii, aidha unaswali unapenda kuuliza au msaada wa ushauri usisite kututafuta.
       Imeandaliwa na ;
            Mwl. Elisante Daudi
       contact: 0759762229









Mhe. RAISI JOHN P. MAGUFURI MFANO WA KUIGWA

MHE.RAISI  MFANO MZURI WA KUIGWA 

                                    Mhe. Raisi JOHN POMBE MAGUFURI
  Tanzania inajivunia kuwa na kiongozi mwenye kujari na kuhimiza maendeleo ya wananchi wake. Napenda kumpongeza Mheshimiwa Raisi wetu kwa kazi kubwa anayoifanya. Kupitia maisha yake ninayomengi ninayoweza kujifunza na hata wewe msomaji wangu Nihaya yafuatayo.
  1. Usimdharau mtu au binadamu mwenzako wakati haujui atakuwa nani siku za mbeleni.
Umesha jiuliza watu waliokuwa wakisoma naye enzi za utoto, huenda walikuwa wakimwona wa kawaida tu laiti wangejua atakuwa nani yamkini wangejari mahitaji yake na kufuatilia maendeleo yake kwa karibu sana.
                 Tazama picha ya mheshimiwa enzi za ujana
  
 2. Pamoja nakuwa hakuna mtu aliyejua atakuwa nani badaye bado yeye hakujidharau kwa kuwa hakuna anajua atakuwa nani bali alijenga hali ya kujiamini na kuthubutu kujaribu kupigania ndoto zake. kwa hilo napenda kukushawishi msomaji wangu usikate tamaa kwa kuwa hakuna anaye kujua wewe ni nani bali angalia ndoto zako kwa kujifunza kwa Raisi wetu mtukufu.
 3. Msimamokatika yale unayo yaamini.
Kati ya vitu ambavyo najifunza kwa Mheshimia ni Msimamo katika yale anayoamini.. Kwa hilo nimependa sana kwani kiongozi hawezi kuwavusha watu anaowaongoza kama hatakuwa na msimamo katika yale anayo yaamini, je,unataka uwe kiongozi bora? Jenga tabia ya kusimamia kile unachokiamini madamu ni kwa ajiri ya manufaa kwa wengi.
  4. Hakubagua kazi. Kiongozi mzuri ni yule ambaye habagui kazi bari atajishughulisha na kazi yoyote madamu inaleta faida mfano, amekuwa mwalimu kwa miaka kadhaa hii inaonesha hakuchagua kazi. Kama unataka kufanikiwa  usiwaze kuanza na mambo makubwa anza na madogo ili uweze kupata makubwa.
   Kwa hayo machache unaweza kuwa umepata ya kujifunza. Tunazidi kumuunga mkono Mheshimiwa kwa kipindi chote cha uongozi wake na tupo tayari kusimamia kauli mbiu ya HAPA KAZI TUUU
       Imeandaliwa na :
                 Mwl. Elisante Daudi
         Contact : 0759762229 










 

Saturday, 21 May 2016

JIPATIE FEDHA SASA

Mambo unayostahili kufahamu kabla ya kuanza biashara Yako

Nimatumaini yangu kuwa ungependa kujikwamua kiuchumi na kufanikisha ndoto yako, watu wengi utawasikia wakilalamika serikali haiwajari naposikia manunguniko hayo huwa najiuliza kwanini unapenda kubebwa na wakati kuna njia rahisi ya kufika katika ndoto zako. wasomi wengi hawana kazi za kufanya  kwa sababu wanapenda kuwaza mambo makubwa mfano kumiliki kampuni lakini  wanasahau kuwa hauwezi kufikia lengo kubwa kama hauna uzoefu na mambo madogo. Leo chukua hatua kwa kuzingatia haya yafuatayo:
  1. Waza kuuza  kile wateja wako wanataka: 
    Usijaribu kufikiri kuagiza yani siangazie tu kile unachotaka. Usipotafakari kuhusu wateja wako,kuna uweza wa kutonunua bidhaa yako. Hakikisha unatafiti soko ili kujua kama huduma au bidhaa yako ni ya maana na nafuu kwa uwezo wa wateja.
  2. Uujue uwezo wako: 
    Angazia sana sana yale unayoyafanya vizuri na uwache mengine. Hustahili kujua majibu yote wala kukusanya maswala yote .Kuwa mwaminifu kwa yale unayoweza kutekeleza na yale usiyomudu kutekeleza. Kumbuka, ni vizuri kuomba msaada iwapo hujui kitu Fulani.
  3. Fanya utafiti wako: 
    Tumia madarasa, hafla au semina, vitabu na kanda ili kujifunza yale unayoweza kabla hujaanza biashara.Kama hujui chochote kuhusu uendeshaji wa biashiara, kuna mafunzo mengine ya malipo ya chini, vitabu na kanda.Jaribu maktaba ya mahali pale unapoishi ama hifadhi ya vitabu, na uulize yale yote usiyoyafahamu kuhusu soko, nguvu na uwezo wako, mahali halisi na yale watu wanataka.
  4. Tegemea juhudi zako: 
    Unahitaji kuwa macho katika bajeti yako, la sivyo, utaishia katika madeni makubwa ama utoweke kutoka biasharani haraka sana. Kama huwezi kupata kila kitu unachokiitaji sasa hivi, wachana nacho na ufikirie zaidi kuhusu mpango wako.
  5. Unda mpango wa mauzo: 
    Hili ndilo swala nyeti la kuwavutia wateja wako. Toa ramani ya jinsi ya kupata wateja wa kutumia bidhaa au huduma yako na namna utakavyowasawishi warejee. Unastahili kujiuza ili watu wakujie.
  6. Huwezi kushughulikia biashara peke yako: 
    Unapokuwa na watu wengi wa kukusaidia na vitu “vidogovidogo”,ndivyo utakavyochukua muda mwingi kunawiri biashara yako. Usiogope kuomba usaidizi na ushauri kutoka kwa rafiki zako na hata watu wa familia

UWEZO WA DAMU YA YESU

FAHAMU UWEZO WA DAMU YA YESU KRISTO
Siku moja usiku nikiwa katika chumba cha hoteli moja hapa hapa nchini, baada ya kutoka kwenye semina ya kiroho; Roho Mtakatifu alisema ndani ya roho yangu kuwa; “Fundisha juu ya Damu ya Yesu Kristo”.
Tangu wakati huo nimekuwa na maombi ya mara kwa mara, nikiomba Roho Mtakatifu anifundishe juu ya Damu ya Yesu Kristo. Nimekuwa nikisoma na kutafakari neno la Mungu linalofundisha juu ya damu ya Yesu Kristo. Ni muda umepita sasa tangu nipate agizo hili. Ndani ya moyo wangu naona ya kuwa muda umefika wa mimi kuanza kuwashirikisha wenzangu yale ambayo tayari yamo ndani yangu ingawa ni machache, juu ya Damu ya Yesu Kristo.
Katika mfulilizo wa somo hili,tutashirikiana juu ya mambo manne tunayopata katika Damu ya Yesu Kristo. Ukweli ni kwamba katika damu ya Yesu Kristo kunapatikana zaidi ya mambo manne nitakayokushirikisha humu; lakini kwa sasa naona nianze na haya manne:-
1. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kuondoa dhambi. Imeandikwa katika kitabu cha 1Yohana 1:9 kuwa; “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata ATUONDOLEE dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.
2. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kupatanisha. Imeandikwa katika kitabu cha Waefeso 2:13-16 kuwa; “Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo. Kwa maana yeye ndiye amanin yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga. Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani. AKAWAPATANISHA wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba”
3. Uzima wa Milele katika Damu ya Yesu Kristo. Imeandikwa katika kitabu cha Yohana 6:53-54 kuwa; “Basi Yesu akawaambia Amini, amini, nawaambieni, msipoula mwili wake mwana wa Adamu nakuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao UZIMA WA MILELE…..”
4. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kutulinda. Imeandikwa katika kitabu cha ufunuo wa Yohana 12:11a kuwa; “Nao wakamshinda (shetani) kwa damu ya mwana-Kondoo….”
Mtihani mkubwa sana kwetu sisi wakristo ni kuyaweka katika matendo yale tunayofahamu katika Biblia. Nakushauri kwa Jina la Yesu Kristo kuwa uwe mtendaji wa neno, na usiwe msomaji tu.
Ni maombi yangu kwa Bwana ya kuwa Roho wa ufahamu wa Bwana atakuwa juu yako. barikiwa sana BY MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE

Friday, 20 May 2016

MKE MWEMA

     MKE MWEMA NI WANAMNA GANI?
     
      



  Vijana wengi wamekuwa wakijiuliza mke mwema au mme mwema ni wa namna gani na anasifa zipi. Hayo yamekuwa ni maswali yao kila kukicha na wengine wamefika hatua ya kuogopa kuanzisha mahusiano au kuingia katika mahusiano kwa sababu ya changamoto mbalimbali ambazo wamekuwa wakiziona kwa wale walio katika mahusiano ,hilo limekuwa shida kwao. Napenda kukufundisha mbinu za kuweza kukusaidia kumtambua mwenzi wako wa maisha na nilipi la kufanya pale unapoziona sifa zile unazozitaka.


                  SIFA ZA MKE NA MME MWEMA

Kila mtu amekuwa na sifa zake mwenyewe lakini tunaweza kuangalia zile za mhimu ambazo unatakiwa kuzitambua.

 1. Mke au Mme unaye mtaka anapaswa awe mcha Mungu.

hii ndiyo sifa kuu na yakuzingatia,kijana kabla ya kuoa au kuolewa ni vizuri atambue kuwa mme au mke atakaye weza kubeba ndoto zake ni yule ambaye anamcha Mungu yani mwenye hofu ya Mungu. kijana wa kiume au wa kike mwenye sifa hii ni mzuri sana tena sana kwa sababu zifuatazo:

     a). mke/mme mwenye hofu ya Mungu hawezi kutoka nje ya ndoa na hawezi kuwa mwenye hasira ya kulipiza na hawezi kukuwazia mabaya hata ukikosana naye atakuwa mwepesi kukusamehe na kusahau.

    b). Hawezi kuwa mwongo, hii ni changamoto ambayo huweza kujitokeza mara kwa mara kati ya wana ndoa lakini kama wakiwa wacha Mungu wataogopa kusema uongo au kujenga mahusiano katika msingi wa uongo. Napenda kushauri wale wanaotegemea kuwa katika mahusiano au waliokwisha ingia waepuke kusema uongo kwani madhara ya uongo ni kupotea kwa uaminifu ndani ya moyo wa yule unayeishi naye au unayetegemea kuishi naye,jarbu kufikiri mke au mme anakuambia anasafiri kwenda kwa shangazi yake lakini unaambiwa hakwenda kwa shangazi alienda kwa rafiki yake utaweza kumwamini? jibu ni hapana lazima moyo utajeruhiwa nakuonya kijana unayetaka kuwa katika mahusiano kwepa kujenga mahusiano katika uongo kwani madhara yake hayafutiki.

    c). Mcha Mungu anakuwa mtii.

Hakuna kitu kizuri wanaume wanapenda kama kupata mke aliye mtii, utii wa mwanamke hupunguza ugomvi na hasira pale panapotokea sitofahamu. Mabinti wengi wamepoteza wachumba wao kwa kukosa utii,ndoa nyingi zina migogoro isiyoisha kwa sababu hakuna roho ya utii miongoni mwa wana ndoa.

    d). Mcha  Mungu haogopi na haoni aibu ya kuomba msamaha.

Neno nisamehe ni nino dogo lakini likikosekana kwa wanandoa ndoa hiyo inakuwa moto, vijana jifunze kuomba msamaha pale unapokuwa umeona kuna mitafaruku imetokea kati yenu.

    


   Ndugu msomaji wangu kuatilia mwendelezo wa somo hili wiki ijayo. Ukiwa na maswali au unahitaji maombi na ushauri wasiliana nami kwa namba 0759762229

       Somo limeandaliwa na :

       Mwl. elisante daudi

Thursday, 19 May 2016

JE UNAJUA SIRI YA MAFANIKIO?

     Kila mtu anapenda kufanikiwa katika maeneo tofauti tofauti ambayo anatamani afanikiwe. Mtu anaweza kutaka afanikiwe katika mambo mbalimbali inaweza kuwa katika Elimu,Biashara,Huduma ya uimbaji, Kuwa mhubiri wa kiwango fulani.Yote hayo hutokana na yale mtu anayowaza na kutamani ambayo wakati mwingine huitwa maono au ndoto. Utasikiwa kila mtu akisema ana ndoto au maono akiwa na mana ya mafanikio ya kuwa na kitu furani katika maisha yake
   Nivizuri na inapendeza kila mtu Kuwaza namna atakavyoweza kufanikiwa katika yale anayotaka na kukusudia  awe nayo.
              MAMBO 6 YA KUKUSAIDIA UFANIKIWE
    1. Penda kuwa nalo hilo unalotaka uwe nalo.
Hauwezi kuwa na kitu usichokipenda, ili uwe na nyumba sharti upende kuwa na nyumba,ili uwe na elimu sharti upende kwenda shule kusoma,ili uwe na biashara sharti upende kuwa na biashara. Kila kitu utakipata pale unapofungua moyo wako kukipenda au kukitaka kitu hicho.
  2. Tafuta elimu juu ya neno hilo unalotaka kufanikiwa
hii ni hatua muhimu sana kwako kwa sababu lazima uwe na ufahamu juu ya hilo jambo unalotaka, linapatikana vipi,je,kuna watu walionalo hilo? je,wenzako wamefanikiwa kwa kiwango gani juu ya hilo? Hayo ni maswali ya muhimu sana
 3. Hesabu gharama ya namna ya kulifanikisha hilo
Hauwezi kukurupuka kujenga nyumba au kufanya biashara kama haujajua kiwango cha fedha utakachotumia kufanikisha hilo au kiyo ndoto yako.
 4.Tafuta marafiki waliokwisha fanikiwa juu ya hilo.
Kwa kupitia hao unaweza pata uzoefu na mbinu walizotumia kufanikiwa,pia unaweza kujifunza maeneo yaliyowahi kuwatatiza wasifanikiwe haraka,
 5. Usiogope changamoto na upinzani.
Mara nyingi tambua hili kila unalowaza si watu wote wanaweza kukufariji na kukuhamasisha nakukufariji wapo watakao kukatisha tamaa na pia changamoto nyingine inaweza kuwa mazingira au ugumu wa kazi,azimia kutokukata tamaa
 6. Jiamini kuwa unaweza kulifikia lengo lako. 
Katika kujiamini ndipo kunamafanikio.

      SOMO: limeandaliwa na
       Mwl   :Elisante Daudi
     CONTACT: +255759762229

FURAHIA MAISHA YA IMANI


Kwa mjibu wa maandiko imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la Mungu.
Waebrania 11:1 inasema "Basi imeni ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo na nibayana ya mambo yasiyo onekana" Ndugu yangu kwa andiko hilo unaweza kuona na kujifunza mambo ya msingi tena siri kubwa sana nayo ni haya yafuatayo:
  1. kuwa na uhakika. hii ni hatua ya msingi sana lazima ujue kuwa kile unachokifikiria kipo na kunawatu ambao wamewahi kufanikiwa kuwa nacho, ukishajenga uhakika huo ndipo wazo lako la kukusudia kuwa na hicho kitu litakuwa imara na utaanza kuchukua hatua za msingi kulipokea neno hilo. Hii ni mhimu uelewe mtu wa Mungu ukijua siri hii utakuwa umefanikiwa. lazima ujue hayo.
  2. Ni miongoni au bayana ya vitu visivyo onekana .
Imani huwa ni wazo linalokuwa ndani yako mfano unawaza kujenga nyumba, kufungua biashara,kuwa na usafiri lakini wakati huo hauna mtaji wa kuwa na kitu hicho lakini kwa kuwa hatua ya kwanza uliweka msingi wa kuamini kwamba hilo uwazalo lipo basi utashangaa nafsi yako inajenga tabia ya kutafuta watu waloifanikuwa kuilpata hilo unalotamani uwe nalo,na utajalibu kfikiri hatua za kuchukua kwa lengo la kufanikiwa kufikia leongo lako. Wakati huo utapaswa kujenga wazo lazima ufanikiwe lazima ufanikiwa kwa hiyo hatua Mungu anacho fanya nikukuongoza na kuitunza afya yako ufikie lengo lako hilo,Mungu ataachia ufunuo halisi namanisha wazo halisi la kuweza kufanikisha wazo lako hilo.
 3. Matarajio.
Jambo la tatu katika andiko hilo ni matarajio yani matokeo ya kile ulicho kiamini na kukisimamia. hii ndiyo hatua ya mwisho au timizo la kusudi la moyo wako, watu wengi huwa wanapenda kuona matokeo ya kile walicho kiamini. Ahimidiwe Mungu aliyetoa tangazo hili kuu kwamba ukiamini yote yanawezekana, ukiamini kwa msingi wa andiko hilo utapata yle unayotaka.
     Nakumbuka miaka ya nyuma najifunza somo hili, niliwaza na kuamua kujenga wazo la kuamini, nilijenga wazo la kumiliki kiwanja katika maeneo ya wilaya yangu kiwanja kizuri nikafanya maombi na kuomba Mungu anipe kiwanja, wakati naomba niliwaza kuamini kuwa Mungu amenipa tayari kiwanja hicho, sikuishia hapo kuamini kuwa maombi yamgu yamejibiwa sawa na maandiko yanavyosema niliamua kuchukua hatua ya kuulizia wapi viwanja vinapatikana na wakati huo sina fedha na sijui fedha nitapata wapi nakumbuka sikukata tamaa bali niliendelea mbele na msimamo wangu wa kutafuta kiwanja, nikaambiwa kuna mtu anacho na kilikuwa kizuri wazo likaja sasa Mungu kiwanja nimepata ndiyo napata wapi fedha,sikukata tamaa nipatana bei na mwenyekiwanja nikiwa njiani natoka kwa mwenye kiwanja nlikutana na mzee mmoja mfanya biashara aliyekuwa ananifahamu akaniuliza mbona unaonekana una mawazo? nikamjibu kunakiwanja jizuri nimepata lakini fedha sina akaniuliza bei nikamwambia akaniambia nitakupatia hiyo fedha ukichukue Haleluya ndipo nilijua MUNGU ana namna tofauti tofauti ya kukupatia yale uliyo yaamini.
                                   MAMBO YA KUZINGATIA
         a . Tambua neno hili kila unaye mwona amefanikiwa au ungetamani kufikia hatua ya maisha aliyo nayo jua kuwa alizaliwa hana kitu hicho kama unavyomwana isipokuwa aliamua kuamini kile alichonacho kuwa kunasiku atakuwa nacho. Chukua hatua ya kuamini.
       b.Tafuta urafiki na wale waliofanikiwa katika lile jambo unalotaka Mungu akupatie,
      c. Jenga tabia ya kununua vitabu au kusoma blog zenye mafundisho juu ya kufanikiwa kupata hicho unachokitaka
     d. Endelea kumwomba Mungu na kusoma maandiko yanayoeleza jambo hilo ni lako.

               SOMO limeandaliwa na:
                        REV. ELISANTE DAUDI
                Contact . +255759762229 

Wednesday, 18 May 2016

Rais Magufuli Atishia Kuwatumbua JIPU Mawaziri Wawili




 Operesheni ya kutumbua majipu ya Rais John Magufuli nusura iwaangukie Mawaziri wawili ambao  pia walikuwa  manaibu  mawaziri katika Serikali ya Awamu ya Nne.


Taarifa kutoka katika chanzo cha kuaminiwa zimeeleza kuwa Rais Magufuli alionesha kutoridhishwa na utendaji wa Mawaziri hao na kuwafokea mbele ya mawaziri wenzao  kwa kuwataja majina katika kikao maalum cha mawaziri kilichofanyika hivi karibuni.
"Ni mazingira ambayo mawaziri hawakuyazoea kwamba Rais anawaambia moja kwa moja kwa majina, anafoka akisema anaweza kuwafukuza wakati wowote.....
"Mawaziri wamezoea mara kwa mara wanapofanya kosa au uzembe wanaonywa kwa staili tofauti, ni kama ya kistaarabu hivi. Sasa huyu bwana mkubwa hana mchezo, aliwataja kabisa, tena mbele ya wenzao ambao walibaki vinywa wazi.

“Wewe (anataja jina la Waziri) na mwenzako (anamtaja jina pia) nitawatumbua,” Chanzo cha gazeti la Rais Mwema kinamkariri Rais Magufuli.
Mawaziri hao ambao ni wabunge wa kuchaguliwa majimboni kwa upande wa Tanzania Bara, wanaongoza wizara nyeti ambazo zinasimamia sekta mtambuka, wizara ambazo zinagusa sehemu ya ahadi za mabadiliko alizonadi Magufuli wakati akigombea urais katika kampeni za mwaka jana.

Chanzo hicho kilieleza kuwa Rais Magufuli aliwaonya pia mawaziri wengine ambao alionesha kutoridhishwa na utendaji wao kwakuwa hawaendani na kasi yake ya kuwaletea wananchi maendeleo.

“Magufuli alitaka atoe mfano kwa mawaziri wengine kwamba wao si watu maalum sana. Kama wanavyotumbuliwa watu wengine na wao pia wanaweza kutumbuliwa,” kiliongeza chanzo hicho

Rais Magufuli aliunda Baraza lake la Mawaziri mwishoni mwa mwaka jana na kuwashauri wasifanye sherehe ya kuteuliwa kwakuwa wakifanya vibaya hatawaonea haya atawaondoa mara moja bila kujali majina yao.

Utendaji wa Rais Magufuli umeendelea kusifiwa kila kona hususan katika kuwawajibisha viongozi wa ngazi zote na kuonesha nia ya dhati ya kuwahudumia watanzania huku akipambana na uzembe na ufisadi.